LATEST NEWS

Thursday, May 4, 2017

Bi Sara Sanga amekemea tabia ya kupotosha tiba na chanjo kwa kuzihusisha na imani za kishirikina.



KATIBU Tawala wa wilaya ya Hanang,Mkoani Manyara Bi Sara Sanga amekemea tabia ya kupotosha tiba na chanjo kwa kuzihusisha na imani za kishirikina.

Katibu Tawala huyo ameyasema hayo kwenye maadhimisho ya wiki ya chanjo duniani iliyofanyika kiwilaya katika Kijiji cha Gitting, wilayani Hanang, Mkoani Manyara.

Akizungumzia kuhusu hali ya chanjo katika wilaya hiyo kwa kipindi cha mwaka 2015 hadi 2017,Bi Sanga amesema kuwa kati ya lengo la kuchanja watoto elfu 65 na 408 kila mwaka lililowekwa na wilaya hiyo,kwa mwaka 2015 wilaya hiyo ilivuka lengo kwa kuchanja watoto 66 elfu  na 7 na 16 sawa na asilimia 102.

Hata hivyo Bi Sanga ametaja matatizo yanayokwamisha zoezi hilo la chanjo katika wilaya hiyo ni uwepo wa asilimia 30 tu ya akina mama wanaojifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya hivyo kuwepo kwa takwimu chache za watoto

No comments:

Post a Comment

Adbox