Timu ya taifa ya soka ya Tanzania
Taifa stars imesafiri kuelekea mwanza kwa matayarisho kabambe huku
kukiwa na wachezaji wapya kikosini kushiriki michezo yajayo.Kati ya hao
ambao Kocha Mkuu Salum Mayanga amewaita, wamo wale aliowatangaza juma
lililopita ambao ni John Bocco, Kevin Sabato pamoja na kinda Athanas
Mdamu ambaye anacheza Alliance ya Mwanza inayoshiriki Ligi Daraja la
Kwanza.
Katika kikosi chake kabla ya kuivaa Rwanda Jumamosi ijayo, wachezaji
wengine ambao Kocha Mayanga amewatangaza leo ni pamoja na Kipa wa
Serengeti Boys – timu ya taifa ya vijana ya Tanzania, Ramadhan Kabwili.
Taifa Stars inajiandaa na mchezo dhidi ya Rwanda unaotarajiwa kufanyika Jumamosi Julai 15, mwaka huu kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN).
Taifa Stars inajiandaa na mchezo dhidi ya Rwanda unaotarajiwa kufanyika Jumamosi Julai 15, mwaka huu kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN).

No comments:
Post a Comment