Rwanda
imeinuka kutoka nafasi ya sita hadi nne kwenye jedwali iliyotolewa
karibuni la umoja wa waendeshaji baiskeli duniani UCI. Ni mafanikio ya
kihistoria kwa kikosi cha wanabaiskeli cha wanaume ya Rwanda baada ya
miaka nyingi ya kutia bidii.
Baada ya taarifa hiyo kutolewa, mwenyekiti wa shirikisho la
wanabaiskeli ya Rwanda Aimable Bayingana alisema kuinuka kwa viwango vya
timu hiyo inatoa motisha ya kufanya vyema zaidi siku za baadaye.
Bayingana alisema wanafurahi kuwa nambari nne barani Afrika, na
kusema kuwa lengo sasa ni kusonga mbele na wala si kurudi nyuma. Hata
hivyo anasema hii inachangamoto zake kwani timu hiyo sasa lazima
ishiriki mashindano mengi ya kimataifa na kutafuta ushindi.
Timu ya Eritrea ilirejea kileleni na kuwa namba moja, mbele ya Morocco ilhali Afrika Kusini inakamilisha jedwali la tatu bora.
No comments:
Post a Comment