Mwimbaji maarufu nchini Tanzania Diamond Platinumz na mkewe Zari Hassan wako katika likizo mjini Mombasa nchini Kenya.
Wawili
hao waliingia katika hoteli ya kifahari ya English Point Marina mjini
humo kwa likizo ya siku tano kulingana
Katika ukurasa wake wa Instagram , Diamond ambaye jina lake
kamili ni Naseeb Abdul alisema kuwa likizo hiyo inalenga kumliwaza
mkewe baada ya kumpoteza mamake Halima Hassan.Wanaandama na meneja wa
Diamond katikja mji huo wa kitalii.
" Mtoto wa watu katoka kwenye matatizo mfululizo msijifanye ni
tamaduni na kulazimisha kila mtu awe kama nyie, eti kutwa nzima
ajifungie nyumbani… Nina siku 5 za kumpetipeti ; leo ndio kwanza'',
alichapisha Diamond katika ukurasa wake wa Instagram.
Hii ni baada
ya Zari kukosolewa na baadhi ya mashabiki kwa kutotumia wakati wake
akimuomboleza mamake na mumewe wa zamani Ivan Ssemwanga.
Siku ya
Jumamosi mwimbaji huyo wa Eneka, alisamabaza picha na video katika
mtandao wake wa Instagram akiwa na mkewe Zari Hassan wakijishebedua.

No comments:
Post a Comment