Sunday, January 7, 2018

JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga limetoa ufafanuzi kuhusu tukio la kuchomwa moto kwa basi la Simba Coach.


N Mwishehe, Globu ya Jamiia Said

Kwa
mujibu wa taarifa zinaeleza basi hilo limechomwa leo na wananchi wenye 
hasira kali baada ya dereva wake kumgonga dereva wa bodaboda. 

Akizungumza
na Michuzi Globu kwa njia ya simu muda huu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa 
Tanga Edward Bukombe amefafanua ni kweli amesikia taarifa za kuchomwa 
moto basi hilo lakini halijachomwa mkoani Tanga kama inavyoelezwa na 
baadhi ya watu.

Amesema baada ya kuona taarifa za kuchomwa basi 
la Simba Coach waliamua kufuatilia lakini wamejiridhisha haikutokea 
kwenye mkoa wao ila basi hilo limechomwa nchini Kenya.

Kamanda 
Bukombe ameiambia Michuzi Globu kuwa basi hiyo ilikuwa inatoka Mombasa 
nchini Kenya na taarifa walizonazo limechomwa huko huko nchini Kenya 
kwani lilikuwa halijaingia kwenye mipaka ya nchi yetu ya Tanzania na 
hasa mkoani Tanga. 

Alipoulizwa iwapo anafahamu namba za basi 
hilo linalodaiwa kuchomwa moto na dereva aliyekuwa analiendesha ,amejibu
wanaendelea kufuatilia kwa polisi wa nchini Kenya na kisha atatoa 
taarifa kuufahamisha umma. 

"Tunaendelea kukusanya taarifa na kwa
kuwa limechomwa huko Kenya tunawasiliana na polisi wa huko ili tuwe na 
uhakika wa taarifa Kamili za tukio hilo.Hatujapata namba za 
basi.Wananchi wasubiri tutaeleza kwa usahihi tutakapokamilisha kupata 
ukweli zinazohusu tukio hilo, "amesema Kamanda Bukombe.

TAARIFA KUCHOMWA MOTO SIMBA MTOTO

Mapema
asubuhi ya leo katika mitandao ya kijamii zilianza kuzagaa picha 
zinazoesha basi linaungua moto, na vyanzo vya moto huo ikawa inaelezwa 
ni wananchi wenye hasira wamechoma moto basi la Simba Coach. 

Taarifa
hizo zikawa zinadai tukio hilo limetokea Mkoa wa Tanga lakini haikuwa 
inaonesha ni wananchi wa eneo gani walioamua kuchoma basi hilo.

Pia
taarifa hiyo imedai basi limochomwa moto kutokana na dereva wake 
kugonga dereva wa pikipiki na hivyo wananchi wakaonesha hasira zao kwa 
kulichoma moto basi hilo.

No comments:

Post a Comment

Adbox