Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foundation tawi la Tanzania Sibtain Meghjee akikabidhi visima hivyo vilivyogharimu sh 21 milioni alisema walisitisha ujenzi wa Msikiti (nyumba ya ibada ) ili watatue kero ya maji kwa kuwapa wananchi huduma ya maji itakayowanufaisha watu zaidi ya 1200 kwa matumizi ya kibinadamu.
Alisema visima vimekabidhiwa ili kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Bi. Fatma AS. mjukuu wa Mtume Mohamed S.A.W.ambaye alifanya kazi kubwa ya kusaidia jamii lakini pia miradi ya kijamii inayofadhiliwa na waumini wa madhahebu ya Shia Ithna Asheri, kwenye maadhimisho hayo ilikabidhiwa huko Kwimba Mwanza na Kondoa mkoani Dodoma na maeneo mengine nchini.

No comments:
Post a Comment