Bunge limeelezwa kuwa, baadhi ya wamiliki wa migodi huwapekua
wafanyakazi hadi sehemu za siri ili kubaini iwapo wameficha madini.
Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Joyce Mukya akiuliza swali leo bungeni
alisema kumekuwa na vitendo vya udhalilishaji kwa wafanyakazi wa
migodini kwa kupekuliwa hadi sehemu za siri na wenye migodi. “Kumekuwa
kunafanyika udhalilishaji mkubwa kwa wafanyakazi, wamekuwa wakikaguliwa
sehemu za siri hasa njia ya haja kubwa, je, Serikali inatuambia nini na
inachukua hatua gani juu ya udhalilishaji huu?” alihoji Mukya. Naibu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana
na Watu wenye Ulemavu, Anthony Mavunde akijibu swali hiyo alisema
malalamiko hayo aliyapata katika mgodi wa TanzaniteOne hivyo
wanayatambua.
Thursday, April 27, 2017
Migodi yalalamikiwa kwa udhalilishaji, yapekua wafanyakazi maungoni
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment