LATEST NEWS

Wednesday, May 3, 2017

Halmashauri ya Arusha mkoani hapa, wamepitisha mwongozo mpya wa mpango mkakati wa serikali

Picha ya Anna MchomeHalmashauri ya  Arusha mkoani hapa, wamepitisha  mwongozo mpya wa mpango mkakati wa serikali, kwa kipindi cha miaka mitano 2016/2020 kupitia Baraza maalumu la madiwani , mpango huo umelenga kupeleka fedha kwenye miradi ya maendeleo ili kutatua kero za wananchi hasa waliopo vijijini.

Akizungumza jana na waandishi wa habari Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Dokta Wilson Mahera alisema kuwa kwa mujibu wa sheria ya mamlaka za serikali za mitaa ya mwaka 1982 kifungu 7 hadi 12 vimetoa uhalali wa uwepo wa serikali za mitaa sambamba na kutimiza wajibu wake wa mpango mkakati (strategic plan)

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri Noah Lembris alisema  baraza kwa pamoja wamefanya maanuzi yenye tija ya kuwapelekea wananchi maendeleo ya kweli bila kujali itikadi ya vyama vyao.

No comments:

Post a Comment

Adbox