LATEST NEWS

Thursday, May 4, 2017

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watanzania wote kutunza miundombinu ya barabara Nchini




Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amewataka watanzania wote kutunza miundombinu yote inayojengwa kwa ajili yao ili kuleta maendeleo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo wakati akikagua ujenzi wa barabara ya Arusha-Holili . Ujenzi huo kwa sasa upo katika awamu ya kwanza yaani barabara ya urefu wa kilomita KM 14 kwa kiwango cha lami kutoka Sakina hadi Tengeru.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu, Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho  Gambo alimueleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,kuwa viongozi wa vijiji wengi wameshiriki kuuza maeneo ya wananchi kiasi kwamba hata serikali inashindwa kupeleka huduma kwa wananchi kwa wakati hususani huduma za kiafya kama zahanati.

Naye Mbunge wa Arumeru Mashariki  Joshua Nasari amuomba Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuweka vivuko viwili vya watu katika eneo la Tengeru na Shangarai.
 

No comments:

Post a Comment

Adbox