LATEST NEWS

Wednesday, June 28, 2017

Mazishi ya walioungua yafanyika Pakistan

Mlipuko huo unatajwa kuwa mkubwa zaidi kwa siku za karibuni nchini humo
Mazishi ya pamoja yamefanyika Pakistan baada ya watu 120 kufariki katika ajali ya moto uliolipuka kutokana na kusuka kwa mpira wa mafuta siku ya Jumapili.

Maombi kwa waliojeruhiwa yalifanyika na kwa waliozikwa pia.

Ulinzi uliimarishwa wakati wa mazishi huku watu hao wakizikwa katika makaburi sita ya pamoja yaliyochimbwa katika kijiji cha Bahawalpur.

Waliozikwa katika makaburi hayo ya pamoja ni wale ambao hawakuweza kufahamika kutokana na kuungua vibaya.

Vipimo zaidi vimechukuliwa na iwapo vitaendana na vya ndugu waliopoteza wapendwa wao wahusika watachukua mwili na kwenda kuuzika tena.

No comments:

Post a Comment

Adbox