Timu ya kriketi ya Kenya ya wachezaji wasiozidi miaka 19 week end iliyopita imefuzu kushiriki kombe la dunia mwaka 2018.
Kenya, ambayo ni taifa la 12 kufuzu kushiriki kombe la dunia
litakaloandaliwa nchini New Zealand kati ya Januari 13 na Februari 3
mwaka 2018, ilinasa tiketi kwa kuibamiza Uganda uwanjani Gymkhana jijini
Nairobi.
Uganda iliingia fainali hizo bila kupoteza mechi hata moja na kujikuta ikipoteza kwa Kenya.
No comments:
Post a Comment