
Spurs iliwalazimu mabingwa hao mara 12 wa Ulaya kupigania sare ya 1-1 katika uwanja wa Bernabeu siku ya Jumanne.
Timu hiyo ya ligi ya Uingereza iliongoza pale Beki wa Madrid Raphael Varane alipolazimika kujifunga kufuatia krosi ya Serge Aurier.
Mabingwa hao wa Uhispania hatahivyo walisawazisha kabla ya kipindi cha kwanza wakati Aurier alipomchezea visivyo Toni Kroos katika eneo hatari na kusababisha penalti iliofungwa na Cristiano Ronaldo.
''Alama moja katika uwanja wa Bernabeu, inaonyesha hatua tulizopiga kama timu'' , alisema Kane mwenye umri wa miaka 24.
''Tunafurahi. Ukweli wni kwamba ijapukuwa walikuwa na fursa tulicheza vizuri na kuwazuia''.
No comments:
Post a Comment