UONGOZI
wa Kiwanda cha mafuta ya makonyo, kilichopo Wawi wilaya ya Chakechake
kisiwani Pemba, umesema moshi unaotoka kwenye kiwanda hicho, hauna
madhara makubwa kwa sasa, baada ya kuwekea kifaa maalum ya kufyonza
kemikali zinazoathiri afya ya mwanadamu.
Akizungumza
na wajumbe wa Tume ya kurekebisha sheria iliokuwa chini ya Mwenyekiti
wake Jaji Mshibe Ali Bakari, Meneja uzalishaji wa kiwanda hicho Habibu
Mohamed Ali, alisema baada ya wahindi kukijenga upya kiwandha hicho,
walifanikiwa kuweka kifaa maalum cha kuondosehea madhara.
Aidha
Meneja huyo uzalishaji, aliwaambia wajumbe wa tume hiyo kuwa, licha
kuwepo kwa kifaa hicho kinachochuja baadhi ya madhara, pia wamefanikiwa
kuurefusha mlingoti unaotoa moshi kwa kwenda juu zaidi.
Ujumbe
wa Tume hiyo ya kurekebisha sheria, ulifika kwenye kiwanda hicho, ili
kuangalia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na usalama wa wafanyakazi na
suala la fidia, wakati huu wakizifanyia mapitio sheria za fidia na ile
ya usalama kazini za mwaka 2005.
Katika
hatua nyengine Meneja huyo uzalishaji kiwandani hapo, aliuhakikishia
ujumbe huo kuwa, wako katika mikakati na mipango ya kuhakikisha kiwanda
hicho, kinazalisha na hakiathiri afya za wafanyakazi wake na wananchi
kwa ujumla.
Mapema
Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar Jaji Mshibe Ali
Bakari, alisema hakuna uhusiano kisheria baina ya kuwepo kiwanda na
kuathiri afya za wafanyakazi na wananchi wengine.
Kwa
upande wao wanasheria wa tume hiyo, waliuomba uongozi wa kiwanda hicho,
kuzielewa sheria za fidia na ile ya usalama kazini, ili kuwafundisha
wafanyakazi wao.
Nao
wafanyakazi wa Kiwanda hicho, walisema hawazifahamu sheria za kazi wala
za fidia, na ikitokezea mtu amepata athari inayotokana na kazi hiyo,
hujitibu kwa gharama zake.
Suleiman
Juma ambae ameanza kazi kiwandani hapo zaidi ya miaka 20 sasa, alisema
aliwahi kuungua na kufikishwa hadi hospitali ya Muhimbili kwa gharama
zake.
“Mimi
sujui kuwa ukipata madhara kazini au kutokana na kazi yako, muajiri
ndie anaepaswa kugharamia matibabu, lazima tuelimisha sheria hizi za
kazi’’,alifafanua.
Mara
baada ya mazungumzo hayo, wajumbe wa tume hiyo walikagua sehemu mbali
mbali za kiwanda hicho kilichojengwa mwaka 1982, ikiwa ni pamoja na eneo
za uzalishaji na shamba la mimea Mtakata lililopo Wawi.
No comments:
Post a Comment